ترجمة معاني سورة الفلق باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation .

Al-Flak


Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,

Na shari ya alivyo viumba,

Na shari ya giza la usiku liingiapo,

Na shari ya wanao pulizia mafundoni,

Na shari ya hasidi anapo husudu.