سورة طه

Ali Muhsin Al - Swahili translation

ترجمة معاني سورة طه باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation

Ali Muhsin Al - Swahili translation

آية رقم 5

Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi.
آية رقم 17

Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?
آية رقم 25

(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,
آية رقم 28

Wapate kufahamu maneno yangu.
آية رقم 41

Na nimekuteuwa kwa ajili ya nafsi yangu.
آية رقم 49

(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?
آية رقم 56

Na hakika tulimwonyesha ishara zetu zote. Lakini alikadhibisha na akakataa.
آية رقم 62

Basi wakazozana kwa shauri yao wenyewe kwa wenyewe, na wakanong'ona kwa siri.

(Firauni) akasema: Oh! Mnamuamini kabla sijakupeni ruhusa? Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliye kufundisheni uchawi. Basi kwa yakini nitakukateni mikono yenu na miguu yenu kwa kutafautisha. Na nitakutundikeni misalabani katika vigogo vya mitende, na hapo kwa yakini mtajua ni nani katika sisi aliye mkali wa kuadhibu na kuiendeleza adhabu yake.

Na hakika Harun alikwisha waambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihanini tu kwa kitu hiki. Na kwa yakini Mola wenu Mlezi ni Arrahmani, Mwingi wa Rehema. Basi nifuateni mimi, na t'iini amri yangu!
آية رقم 122

Kisha Mola wake Mlezi akamteuwa, naye akamkubalia toba yake, naye akamwongoa.
آية رقم 126

(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo vivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika leo unasahauliwa.
آية رقم 129

Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutoka kwa Mola wako Mlezi na muda ulio wekwa, bila ya shaka inge fika adhabu (hapa hapa).
تقدم القراءة