ترجمة معاني سورة ص باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
آية رقم 1
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Sad
S'ad, Naapa kwa Qur'ani yenye mawaidha.
آية رقم 2
ﭗﭘﭙﭚﭛﭜ
ﭝ
Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani
آية رقم 3
Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita.
آية رقم 4
Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.
آية رقم 5
Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.
آية رقم 6
Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa.
آية رقم 7
Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.
آية رقم 8
Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu.
آية رقم 9
Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?
آية رقم 10
Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!
آية رقم 11
ﯟﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa.
آية رقم 12
Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo.
آية رقم 13
Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi.
آية رقم 14
Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu.
آية رقم 15
Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.
آية رقم 16
Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu.
آية رقم 17
Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia.
آية رقم 18
Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye.
آية رقم 19
ﭦﭧﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.
آية رقم 20
ﭭﭮﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hikima, na kukata hukumu.
آية رقم 21
Na je! Imekufikia khabari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani?
آية رقم 22
Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa.
آية رقم 23
Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno.
آية رقم 24
Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia.
آية رقم 25
Basi tukamsamehe kwa hayo. Naye kwa hakika anao mkaribisho mkubwa na marejeo mazuri kwetu.
آية رقم 26
Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa katika nchi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanao ipotea Njia ya Mwenyezi Mungu wakaiacha, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.
آية رقم 27
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utao wapata.
آية رقم 28
Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu?
آية رقم 29
Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.
آية رقم 30
Na Daudi tukamtunukia Suleiman. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia.
آية رقم 31
ﮅﮆﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
Alipo pelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;
آية رقم 32
Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma.
آية رقم 33
(Akasema:) Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.
آية رقم 34
Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu.
آية رقم 35
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji.
آية رقم 36
Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika.
آية رقم 37
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Na tukayafanya mashet'ani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.
آية رقم 38
ﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
Na wengine wafungwao kwa minyororo.
آية رقم 39
Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hisabu.
آية رقم 40
ﯷﯸﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.
آية رقم 41
Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shet'ani amenifikishia udhia na adhabu.
آية رقم 42
(Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa.
آية رقم 43
Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iwe kumbusho kwa watu wenye akili.
آية رقم 44
Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu.
آية رقم 45
Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu walio kuwa na nguvu na busara.
آية رقم 46
ﭶﭷﭸﭹﭺ
ﭻ
Sisi tumewakhusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera.
آية رقم 47
ﭼﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora.
آية رقم 48
Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora.
آية رقم 49
Huu ni ukumbusho. Na hakika wachamngu wana marudio mazuri.
آية رقم 50
ﮔﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Bustani za milele zitazo funguliwa milango yao kwa ajili yao.
آية رقم 51
Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji.
آية رقم 52
ﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao.
آية رقم 53
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.
آية رقم 54
Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.
آية رقم 55
ﯗﯘﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa;
آية رقم 56
ﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia.
آية رقم 57
ﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!
آية رقم 58
ﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Na adhabu nyenginezo za namna hii.
آية رقم 59
Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.
آية رقم 60
Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa!
آية رقم 61
Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni.
آية رقم 62
Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu?
آية رقم 63
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu hayawaoni?
آية رقم 64
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni.
آية رقم 65
Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu,
آية رقم 66
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
آية رقم 67
ﭿﮀﮁﮂ
ﮃ
Sema: Hii ni khabari kubwa kabisa.
آية رقم 68
ﮄﮅﮆ
ﮇ
Ambayo nyinyi mnaipuuza.
آية رقم 69
Sikuwa na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana.
آية رقم 70
Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri.
آية رقم 71
Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.
آية رقم 72
Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.
آية رقم 73
ﮯﮰﮱﯓ
ﯔ
Basi Malaika wakat'ii wote pamoja.
آية رقم 74
ﯕﯖﯗﯘﯙﯚ
ﯛ
Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.
آية رقم 75
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?
آية رقم 76
Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.
آية رقم 77
ﯷﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.
آية رقم 78
ﯽﯾﯿﰀﰁﰂ
ﰃ
Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.
آية رقم 79
ﰄﰅﰆﰇﰈﰉ
ﰊ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe.
آية رقم 80
ﰋﰌﰍﰎ
ﰏ
Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,
آية رقم 81
ﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
آية رقم 82
ﰕﰖﰗﰘ
ﰙ
Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote,
آية رقم 83
ﰚﰛﰜﰝ
ﰞ
Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio khitariwa.
آية رقم 84
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Akasema: Haki! Na haki ninaisema.
آية رقم 85
Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao.
آية رقم 86
Sema (Ewe Mtume): Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu.
آية رقم 87
ﭩﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.
آية رقم 88
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda.
تقدم القراءة