إِنَّمَا ٱلۡمُؤۡمِنُونَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ ثُمَّ لَمۡ يَرۡتَابُواْ وَجَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلصَّـٰدِقُونَ
Hakika Waumini ni wale walio muamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake tena wasitie shaka kabisa, na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali yao na nafsi zao. Hao ndio wakweli.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ni kwamba Waumini ni wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafuata sheria Zake kivitendo, kisha wasiwe na shaka katika Imani yao, na wakatoa raali yao mazuri na roho zao kwa kupigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, kumtii Yeye na kutafuta radhi Zake, basi hao ndio wakweli katika Imani Yao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس