إِن يَثۡقَفُوكُمۡ يَكُونُواْ لَكُمۡ أَعۡدَآءٗ وَيَبۡسُطُوٓاْ إِلَيۡكُمۡ أَيۡدِيَهُمۡ وَأَلۡسِنَتَهُم بِٱلسُّوٓءِ وَوَدُّواْ لَوۡ تَكۡفُرُونَ
Wakikuwezeni wanakuwa maadui zenu, na wanakukunjulieni mikono yao na ndimi zao kwa uovu. Na wanapenda muwe makafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wakiwapatia nafasi nyinyi hao mnaowapenda kwa siri watawapiga vita na watanyosha mikono yao kwenu, wawaue nyinyi na wawateke, na pia ndimi zao, wawatukane nyinyi na wawatusi, na wao walitamani, kwa hali yoyote, lau nyinyi mlikanusha kama wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس