يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ جَٰهِدِ ٱلۡكُفَّارَ وَٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱغۡلُظۡ عَلَيۡهِمۡۚ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Ewe Nabii! Pambana na makafiri na wanaafiki, na kuwa mgumu kwao! Na makaazi yao ni Jahannamu. Na hayo ni marejeo mabaya.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ewe Nabii! Pigana jihadi na wale waliouonyesha ukafiri waziwazi na wakautangaza, na pigana nao kwa upanga, na pigana jihadi na wale waliouficha ukafiri na kuufinika kwa hoja na kwa kusimamisha hukumu za Sheria na vitambulisho vyaa Dini. Na utumie ukali na ugumu katika kupigana jihadi na makundi mawili hayo. Na makazi yao ambayo watakwenda kukaa huko Akhera ni moto wa Jahanamu. Na ni marejeo maovu mno hayo watakayoyarejea!
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس