ترجمة معاني سورة المطفّفين باللغة السواحلية من كتاب Ali Muhsin Al - Swahili translation
آية رقم 1
ﯖﯗ
ﯘ
Al-Mutaffifin
Ole wao hao wapunjao!
آية رقم 2
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
آية رقم 3
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
آية رقم 4
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
آية رقم 5
ﭑﭒ
ﭓ
Katika Siku iliyo kuu,
آية رقم 6
ﭔﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
آية رقم 7
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
آية رقم 8
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Unajua nini Sijjin?
آية رقم 9
ﭦﭧ
ﭨ
Kitabu kilicho andikwa.
آية رقم 10
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
آية رقم 11
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
آية رقم 12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
آية رقم 13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
آية رقم 14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
آية رقم 15
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
آية رقم 16
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Kisha wataingia Motoni!
آية رقم 17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
آية رقم 18
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
آية رقم 19
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
آية رقم 20
ﮭﮮ
ﮯ
Kitabu kilicho andikwa.
آية رقم 21
ﮰﮱ
ﯓ
Wanakishuhudia walio karibishwa.
آية رقم 22
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
آية رقم 23
ﯙﯚﯛ
ﯜ
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
آية رقم 24
ﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
آية رقم 25
ﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
آية رقم 26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
آية رقم 27
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
آية رقم 28
ﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
آية رقم 29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
آية رقم 30
ﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
آية رقم 31
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
آية رقم 32
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
آية رقم 33
ﰕﰖﰗﰘ
ﰙ
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
آية رقم 34
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
آية رقم 35
ﭘﭙﭚ
ﭛ
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
آية رقم 36
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
تقدم القراءة