ترجمة معاني سورة المطفّفين باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﯖﯗ
ﯘ
Adhabu kali ni ya wale wanaopunja vipimo vya vibaba na mezani.
آية رقم 2
ﯙﯚﯛﯜﯝﯞ
ﯟ
Ambao wakinunua kwa watu cha kupimwa kwa vibaba au kwa mizani hujikamilishia wao wenyewe.
آية رقم 3
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Na wakiwauzia watu kinachouzwa kwa vibaba au mizani wanapunguza vipimo.
آية رقم 4
ﯦﯧﯨﯩﯪ
ﯫ
Basi itakuwaje hali ya yule anayeiba na kupunja katika vipimo vyote hivyo, au yule anayeiba katika vipimo hivyo na huku awapunja watu vitu vyao? Hakika huyo yuwastahiki mateso zaidi kuliko wapunguzaji wa vipimo vya vibaba na mizani. Kwani hawaamini wale wapunjaji ya kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mwenye kuwafufua na kuwahesabu juu ya vitendo vyao.
آية رقم 5
ﭑﭒ
ﭓ
katika Siku itakapokuwa na kitisho?
آية رقم 6
ﭔﭕﭖﭗﭘ
ﭙ
Siku watakaposimama watu mbele ya Mweyezi Mungu ili Awahesabu kwa machache na mengi walioyatenda, hali ya kuwa wao Siku Hiyo ni wenye kumnyenyekea Mwenyezi Mungu, Mlezi wa viumbe vyote.
آية رقم 7
ﭚﭛﭜﭝﭞﭟ
ﭠ
Hakika marejeo ya watu waovu na makazi yao yatakuwa katika hali ya dhiki.
آية رقم 8
ﭡﭢﭣﭤ
ﭥ
Na ni kipi kinachokujulidha dhiki hii ni ipi?
آية رقم 9
ﭦﭧ
ﭨ
Hakika hiyo itakuwa ni jela ya kudumu na adhabu iliyo na uchungu. Penye jela hiyo ni pale walipoandikiwa kuwa watakwenda. Wameandikiwa na imepitishwa. Hapana kitakachozidishwa wala kupunguzwa.
آية رقم 10
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Adhabu kali Siku Hiyo ni ya wale wenye kukanusha.
آية رقم 11
ﭭﭮﭯﭰ
ﭱ
Wale ambao wanakanusha kuwako tukio la Siku ya Malipo.
آية رقم 12
Na wala haikanushi Siku Hiyo isipokuwa kila dhalimu mwenye madhambi mengi.
آية رقم 13
Anaposomewa aya za Qur’ani, husema, «Hizi ni hadithi za urongo za watu wa kale.» Mambo yalivyo si kama wanavyodai!
آية رقم 14
Bali hayo ni maneno ya Mwenyezi Mungu na Wahyi Wake kwa Mtume Wake.
آية رقم 15
ﮍﮎﮏﮐﮑﮒ
ﮓ
Na hakika zimezibwa nyoyo zao zikawa hazimkubali Mwenyezi Mungu. Na kile kilichoziziba nyoyo hizo ni kufinikwa na wingi wa madhambi wanayoyafanya. Mambo hayako kama vile wanavyodai makafiri! Bali hakika wao, Siku ya Kiyama watazibwa wasimuone Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda. Aya hii ni ushahidi kwamba Waumini watamuona Mola Wao Peponi.
آية رقم 16
ﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Kisha hakika hao makafiri ni wenye kuingia Motoni, na wataziona na kuzihisi dharubu zake.
آية رقم 17
Kisha wataambiwa,»Haya ndiyo malipo ya yale ambayo mlikuwa mnayakanusha.»
آية رقم 18
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Ni kweli kabisa kwamba kitabu cha watu wema, nao ni wachamungu, kiko katika ngazi za juu Peponi.
آية رقم 19
ﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Na ni kipi kinachokujulisha ni zipi hizi ngazi za juu?
آية رقم 20
ﮭﮮ
ﮯ
Ni kitabu cha watu wema kilichopitishwa mambo yake, hakizidishwi kitu humo wala hakipunguzwi.
آية رقم 21
ﮰﮱ
ﯓ
Wanayatazama yaliyomo ndani yake Malaika waliokurubishwa, wa kila mbingu.
آية رقم 22
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
Hakika wale wenye ukweli na kufuata amri za Mwenyezi Mungu watakuwa Peponi wnaneemeka,
آية رقم 23
ﯙﯚﯛ
ﯜ
juu ya viti vya fahari wanamwangalia Mola wao na wanaangalia yale waliyoandaliwa miongoni mwa kheri nyingi.
آية رقم 24
ﯝﯞﯟﯠﯡ
ﯢ
Unaonekana katika nyuso zao mng’aro wa neema.
آية رقم 25
ﯣﯤﯥﯦ
ﯧ
Watanyweshwa tembo safi, lililotengezewa vyombo kwa ustadi na mwishowe kuna harufu ya miski.
آية رقم 26
Katika kuzipata neema hizo, nawashindane wenye kushindana.
آية رقم 27
ﯰﯱﯲ
ﯳ
Na kinywaji hiki, mchanganyo wake watokana na chemchemi iliyoko Peponi linalojulikana, kwa ubora wake, kwa jina la Tasnīm.
آية رقم 28
ﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Hiyo ni chemchemi iliyoandaliwa wale waliokurubishwa kwa Mwenyezi Mungu na watajiburudisha nayo.
آية رقم 29
Hakika wale waliotenda maovu walikuwa duniani wakiwacheza shere Waumini.
آية رقم 30
ﰂﰃﰄﰅ
ﰆ
Na wanapowapitia wanakonyezana kwa kuwakejeli.
آية رقم 31
ﰇﰈﰉﰊﰋﰌ
ﰍ
Na wnaporudi, hawa waovu, kwa watu wao na jamaa zao, huwa na vihunzi na wao kwa kuwafanyia maskhara Waumini.
آية رقم 32
ﰎﰏﰐﰑﰒﰓ
ﰔ
Na hawa makafiri wanapowaona Maswahaba wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wamefuata uongofu, huwa wakisema, «Hakika hawa wamepotea kwa kumfuata Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
آية رقم 33
ﰕﰖﰗﰘ
ﰙ
Na wala waovu hawa hawakutumwa wawe ni wachunguzi kwa Maswahaba na Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
آية رقم 34
ﭑﭒﭓﭔﭕﭖ
ﭗ
Basi Siku ya Kiyama wale waliomkubali Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakafanya vitendo vinavyolingana na sheria Zake, watawafanyia maskhara makafiri kama makafiri walivyokuwa wakiwafanyia mashara duniani.
آية رقم 35
ﭘﭙﭚ
ﭛ
Juu ya viti vya fahari, watakuwa Waumini wanaangalia yale Aliyowapa Mwenyezi Mungu miongoni mwa mambo matukufu na neema, wakiwa Peponi. Na neema kubwa ya zote ni kuangalia Uso wa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
آية رقم 36
ﭜﭝﭞﭟﭠﭡ
ﭢ
Je, wamelipwa makafiri, pindi watakapo kufanyiwa hayo, malipo muwafaka na yale waliyoyafanya duniani ya shari na madhambi?
تقدم القراءة