ترجمة معاني سورة الماعون باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Je, waiona hali ya yule ambaye akanusha kufufuliwa na kulipwa?
آية رقم 2
ﭫﭬﭭﭮ
ﭯ
Huyo ndiye yule anayemkaripia yatima kwa nguvu akimnyima haki yake kwa sababu ya ususuavu wa moyo wake.
آية رقم 3
ﭰﭱﭲﭳﭴ
ﭵ
Na wala hawahimizi wengine kulisha masikini. Vipi yeye mwenyewe atamlisha?.
آية رقم 4
ﭶﭷ
ﭸ
Basi adhabu kali itawafikia wenye kusali,
آية رقم 5
ﭹﭺﭻﭼﭽ
ﭾ
ambao wameghafilika na Swala zao: hawazisimamishi kama ipasavyo wala hawazisali kwa nyakati zake.
آية رقم 6
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Ambao huonyesha watu amali zao za kheri kwa njia ya ria.
آية رقم 7
ﮃﮄ
ﮅ
Na wanakataa kuwaazima watu vitu ambavyo hawadhuriki kwa kuviazima, kama vyombo vya kutumia na vinginevyo. Wao hawakujifanyia wema nafsi zao kumuabudu Mola wao wala hawakuwafanyia wema viumbe Vyake.
تقدم القراءة