ترجمة معاني سورة عبس باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﭑﭒ
ﭓ
Yalidhihiri mabadiliko na mkunjiko katika uso wa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
آية رقم 2
ﭔﭕﭖ
ﭗ
na akapa nyongo kwa sababu ya kwamba Abdallah bin Ummi Maktum alimjilia akitaka aelekezwe. Na alikuwa Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ameshughulika kuwalingania miamba wa Kikureshi katika Uislamu.
آية رقم 3
ﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
Ni kitu gani kinakufanya wewe ujue uhakika wa jambo lake? Kwani huenda ikawa, kwa kuuliza kwake, nafsi yake itatakasika na kusafika.
آية رقم 4
ﭝﭞﭟﭠ
ﭡ
Au pengine apate mazingatio zaidi na kutishika.
آية رقم 5
ﭢﭣﭤ
ﭥ
Basi yule alijyejitosheleza na kutouhitajia uongozi wako,
آية رقم 6
ﭦﭧﭨ
ﭩ
wewe ndiye unayemjali na wapulikiza maneno yake.
آية رقم 7
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Na ni kitu gani kinachokupa jukumu kwako iwapo hakusafika na ukafiri wake?
آية رقم 8
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Ama yule ambaye amekuwa na pupa la kukutana na wewe,
آية رقم 9
ﭴﭵ
ﭶ
na huku anamuogopa Mwenyezi Mungu asiwe na kasoro katika kupata uongofu,
آية رقم 10
ﭷﭸﭹ
ﭺ
wewe unampuuza. Ilivyotakikana ufanye si kama ulivyofanya, ewe Mtume.
آية رقم 11
ﭻﭼﭽ
ﭾ
Hakika Sura hii ni mawaidha kwako na kwa kila anayetaka kuwaidhika.
آية رقم 12
ﭿﮀﮁ
ﮂ
Basi atakaye atamkumbuka Mwenyezi Mungu na kumtaja na atafuata Wahyi Wake.
آية رقم 13
ﮃﮄﮅ
ﮆ
Wahyi huu, nao ni Qur’ani, uko katika kurasa zilizotukuzwa,
آية رقم 14
ﮇﮈ
ﮉ
zenye kuheshimiwa, zenye cheo cha juu,
آية رقم 15
ﮊﮋ
ﮌ
zilizosafishwa na uchafu, uongezaji na upunguzaji.
آية رقم 16
ﮍﮎ
ﮏ
Zilizoko mikononi mwa Malaika waandishi, mabalozi kati ya Mwenyezi Mungu na viumbe Wake, wenye maumbile mema, tabia zao ni nzuri na njema na pia matendo yao.
آية رقم 17
ﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Amelaaniwa mtu kafiri na ataadhibiwa. Ni uovu ulioje wa ukafiri wake kwa Mola wake!
آية رقم 18
ﮕﮖﮗﮘ
ﮙ
Kwani hajui ni kwa kitu gani Mwenyezi Mungu Alimuumba kwacho mwanzo wake?
آية رقم 19
ﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
Mwenyezi Mungu Alimuumba kwa maji machache, nayo ni manii. Akayakadiria miongo yake.
آية رقم 20
ﮟﮠﮡ
ﮢ
Kisha Akambainishia njia ya kheri na ya shari.
آية رقم 21
ﮣﮤﮥ
ﮦ
Kisha humkosesha uhai, na Amemuekea mahali pa kuzikiwa.
آية رقم 22
ﮧﮨﮩﮪ
ﮫ
Kisha Akitaka Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na sifa mbaya, Atamhuisha na kumfufua baada ya kifo chake, kwa ajili ya kuhesabiwa na kulipwa.
آية رقم 23
ﮬﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Mambo siyo kama yale anayoyasema kafiri na anayoyafanya. Bado hajatakeleza Aliyomuamrisha kwayo Mwenyezi Mungu katika kuamini na kutenda wema kwa kumtii.
آية رقم 24
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na azingatie binadamu, vipi Mwenyezi Mungu Amekiumba chakula chake ambacho ndicho kinachoendeleza maisha yake?
آية رقم 25
ﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Aone kwamba Sisi Tumeyamimina maji ya mvua juu ya ardhi kwa wingi.
آية رقم 26
ﯝﯞﯟﯠ
ﯡ
Kisha Tumeipasua ardhi kwa Tulivyo vitoa kutoka humo miongoni mwa mimea tofauti.
آية رقم 27
ﯢﯣﯤ
ﯥ
Tukaotesha humo nafaka
آية رقم 28
ﯦﯧ
ﯨ
na zabibu, na nyasi za wanyama.Na mizaituni na mitende.
آية رقم 29
ﯩﯪ
ﯫ
Na mabustani yenye miti mikubwa.
آية رقم 30
ﯬﯭ
ﯮ
Na matunda
آية رقم 31
ﯯﯰ
ﯱ
na ndisha.
آية رقم 32
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Mnajistareheshea kwazo, nyinyi na wanyama wenu.
آية رقم 33
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Utakapokuja Ukelele wa Siku ya Kiyama, ambao utayatia uziwi, kwa kitisho chake, masikizi.
آية رقم 34
ﯺﯻﯼﯽﯾ
ﯿ
Siku mtu atakapomkimbia, kwa kitisho cha Siku Hiyo, nduguye
آية رقم 35
ﰀﰁ
ﰂ
na babake na mamake na
آية رقم 36
ﰃﰄ
ﰅ
mkewe na wanawe.
آية رقم 37
ﰆﰇﰈﰉﰊﰋ
ﰌ
Kila mmoja Siku Hiyo, atakuwa na jambo litakalomzuia asishughulike na mwingine.
آية رقم 38
ﰍﰎﰏ
ﰐ
Nyuso za wenye neema, Siku Hiyo, zitakuwa ni zenye kung’ara,
آية رقم 39
ﰑﰒ
ﰓ
zenye furaha na nderemo.
آية رقم 40
ﰔﰕﰖﰗ
ﰘ
Na nyuso za watu wa Motoni zitakuwa na giza,
آية رقم 41
ﭑﭒ
ﭓ
nyeusi, zafinikwa na unyonge.
آية رقم 42
ﭔﭕﭖﭗ
ﭘ
Hao wenye kusifika na sifa hiyo ndiwo wale waliozikufuru neema za Mwenyezi Mungu na wakazikanusha aya zake na wakayakeuka Aliyoyaharamisha kwa kutenda maovu na kukiuka mipaka.
تقدم القراءة