ترجمة معاني سورة الضحى باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﮉ
ﮊ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
آية رقم 2
ﮋﮌﮍ
ﮎ
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
آية رقم 3
ﮏﮐﮑﮒﮓ
ﮔ
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
آية رقم 4
ﮕﮖﮗﮘﮙ
ﮚ
Na Nyumba ya Akhera ni bora kwako kuliko nyumba ya ulimwengu.
آية رقم 5
ﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
آية رقم 6
ﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
آية رقم 7
ﮥﮦﮧ
ﮨ
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
آية رقم 8
ﮩﮪﮫ
ﮬ
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
آية رقم 9
ﮭﮮﮯﮰ
ﮱ
Basi yatima usimtende ubaya.
آية رقم 10
ﯓﯔﯕﯖ
ﯗ
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
آية رقم 11
ﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
تقدم القراءة