سورة الضحى

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة الضحى باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa dhuha, na uliokusudiwa ni wakati wa mchana mzima.
آية رقم 2
Na kwa usiku utuliapo na viumbe na likashadidi giza lake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Atakacho katika viumbe vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa kwa asiyekuwa Muumba wake. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
آية رقم 3
Hakukuwacha Mola wako, ewe Mtume, wala Hakukuchukia kwa kuchelewesha kukuteremshiaWahyi.
آية رقم 5
Na Atakupa Mola wako, ewe Mtume, neema ya kila sampuli uridhike.
آية رقم 6
Kwani Hakukupata, kabla ya hapo, kuwa ni yatima Akakukusanya na kukutunza.
آية رقم 7
Na Akakupata hujui Kitabu wala Imani, Akakufundisha yale amabayo ulikuwa huyajui na akakuafikia kufanya amali bora?
آية رقم 8
Na Akakupata masikini, Akakuletea riziki yako na Akakutajirisha kwa kutosheka na kusubiri?
آية رقم 10
Na muombaji usimkaripie, bali mlishe na umtimizie haja yake.
آية رقم 11
Na ama neema ya Mola wako Aliyokuneemesha nayo izungumze.
تقدم القراءة