سورة البلد

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة البلد باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mji huu mtakatifu wa Makkah.
آية رقم 3
Na Anaapa kwa mzazi wa wanaadamu, ambaye ni Ādam, amani imshukie, na kilichozalikana na yeye.
آية رقم 4
Hakika Tumemuumba binadamu katika usumbufu na shida za kilimwengu.
آية رقم 5
Kwani anadhani kwa mali aliyoyakusanya kuwa Mwenyezi Mungu Hatakuwa na uwezo juu yake?
آية رقم 6
Huwa akisema kwa kujigamba: «Nimetumia mali mengi.»
آية رقم 7
Kwani anadhani, kwa kitendo chake hiko, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kushinda, Hamuoni wala hatamhesabu juu ya kubwa na dogo?
آية رقم 9
ulimi na midomo miwili ya kusemea
آية رقم 10
na kumfafanulia njia mbili: ya kheri na ya shari?
آية رقم 11
Basi ajiepushe na janga la Akhera kwa kutoa mali yake ili aokoke.
آية رقم 12
Ni kitu gani kilichojulisha ni lipi hilo janga la Akhera na ni mambo gani yenye kusaidia kujiepusha nalo?
آية رقم 13
Ni kuacha huru shingo iliyoamini kuikomboa na utumwa.
آية رقم 15
yatima mwenye ujamaa, ili ipatikane fadhila ya sadaka na ya kuunga kizazi,
Kisha akawa, baada ya kufanya amali njema zilizotajwa, ni miongoni mwa waliotakasa Imani yao kwa Mwenyezi Mungu, wakausiana kusubiri juu ya kumtii Mwenyezi Mungu kwa kufuata maamrisho Yake na kujiepusha na vitendo vya kumuasi na wakausiana kuwahurumia viumbe.
آية رقم 18
Wenye kufanya hayo ndiwo watu wa kulia ambao watapelekwa Siku ya Kiyama upande wa kulia kuelekea Peponi.
آية رقم 19
Na wale waliokanusha Qur’ani ndio ambao watapelekwa, Siku ya Kiyama, upande wa kushoto kuelekea Motoni.
آية رقم 20
Malipo yao ni Moto wa Jahanamu wenye kuwafinika na kuwaziba.
تقدم القراءة