سورة الشمس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة الشمس باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa jua na mchana wake na mwangaza wake wa asubuhi.
آية رقم 2
Na kwa mwezi unapolifuata wakati wa kucha na kutwa.
آية رقم 3
Na kwa mchana unapoliondoa giza na kulifunua.
آية رقم 4
Na kwa usiku unapoifinika ardhi ikawa giza.
آية رقم 5
Na kwa mbingu na kujengeka kwake kiimara.
آية رقم 7
Na kwa kila nafsi na namna Mwenyezi Mungu alivyoikamilisha umbo lake ili itekeleze kazi iliyoumbiwa nayo.
آية رقم 8
Akaibainishia njia ya shari na njia ya kheri.
آية رقم 10
Na ameingia kwenye hasara mwenye kuitia nafsi yake kwenye maasia.
آية رقم 11
Kabila la Thamūd lilimkanusha Nabii wake kwa kuvama kwenye uasi.
آية رقم 12
Pindi walipotoka wabaya zaidi wa kabila hilo kumchinja Ngamia. Mtume wa Mwenyezi Mungu’ Ṣāliḥ, amani imshukie,
آية رقم 13
akawaambia: «Tahadharini kumgusa kwa ubaya ngamia ambaye ni miujiza ilioletwa na Mwenyezi Mungu kwenu inayoonyesha ukweli wa Nabii wenu, na msizuie kinywaji chake. Yeye ana siku yake ya kunywa na nyinyi mna siku yenu maalumu ya kunywa.» Hilo likawa zito kwao.
آية رقم 14
Wakamkanusha na kulipuza onyo lake wakamchinja.Mola wao Akawafinika kwa adhabu, akaisawazisha juu yao na hakuna aliyeweza kuponyoka.
آية رقم 15
Wala Haogopi, Mwenye uwezo uliotukuka, athari ya adhabu kali Aliywateremshia.
تقدم القراءة