سورة الأعلى

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة الأعلى باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Takasa Jina la Mola wako Aliyetukuka na kuepukana na mshirika na kila sifa pungufu kwa namna inayonasibiana na utukufu Wake na utakatifu Wake.
آية رقم 2
Aliyeumba viumbe Akalitengeneza umbo lao na kulifanya zuri.
آية رقم 3
Na Aliyekadiria kila kitu na kukipeleka njia inayonasibiana nacho.
آية رقم 4
Na Aliyeotesha nyasi mbiti zenye rangi ya kijani,
آية رقم 5
Akazifanya baadaye kuwa kavu zilizobadilika rangi.
آية رقم 6
Tutakusomea, ewe Mtume, hii Qur’ani kisomo ambacho hutakisahau.
Isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Ataka usahau kwa hekima na maslahi anayoyajua Yeye. Kwani Yeye ni Mjuzi wa yaliyo wazi na yaliyofichika, ya maneno na ya vitendo.
آية رقم 8
Tutakufanyia mapesi mambo yako yote; miongoni mwayo ni kukusahilishia kubeba majukumu ya utume na kuifanya nyepesi Dini uliyokuja nayo.
آية رقم 9
Basi wawaidhie kaumu zako, ewe Mtume, kwa namna tulivyokutayarishia ufanye kwenye wahyi ulioletewa, uwaongoze njia yenye kheri na wao na uwahusu kwa mawaidha yako wale wanaotarajiwa kuwaidhika nayo. Wala usijisumbue kuwashauri wale ambao mawidha hayawaathiri isipokuwa kuwatia ujeuri na kuwafanya wayakimbie.
آية رقم 10
Atanufaika kwa mawaidha anayemcha Mola wke,
آية رقم 11
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
آية رقم 12
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
آية رقم 13
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
آية رقم 14
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
آية رقم 15
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
آية رقم 16
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
آية رقم 17
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
آية رقم 18
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
آية رقم 19
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
تقدم القراءة