ترجمة معاني سورة المرسلات باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﮑﮒ
ﮓ
Anaapa Mwenyezi Mungu kwa upepo unapovuma kwa mfululizo, huu baada ya huu.
آية رقم 2
ﮔﮕ
ﮖ
Na kwa upepo wenye kuvuma kwa ukali wenye kuangamiza.
آية رقم 3
ﮗﮘ
ﮙ
Na kwa Malaika waliopewa jukumu la mawingu, wakawa wayapeleka pale anapotaka Mwenyezi Mungu.
آية رقم 4
ﮚﮛ
ﮜ
Na kwa Malaika wanaoshuka, kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
آية رقم 5
ﮝﮞ
ﮟ
na amri zinazopambanua baina ya haki na batili na halali na haramu.
آية رقم 6
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Na kwa Malaika wanaoupokea wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuuteremsha kwa Manabii Wake, unaowapa viumbe wake udhuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu na pia onyo kutoka Kwake, ili watu wasiwe na hoja.
آية رقم 7
ﮤﮥﮦ
ﮧ
Hakika jambo la Kiyama mnaloahidiwa pamoja na lile la kuhesabiwa na kulipwa ni lenye kuwa hapana shaka.
آية رقم 8
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Basi nyota zitakapofutwa na mwangaza wake ukaondoka,
آية رقم 9
ﮬﮭﮮ
ﮯ
na mbingu zitakapopasuka,
آية رقم 10
ﮰﮱﯓ
ﯔ
na majabali yatakapopeperuka na kukueanea huku na kule na yakawa ni mapepe yanayorushwa na upepo,
آية رقم 11
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Na Mitume watapowekewa wakati na muda wa baina yao na ummah wao na kusemwe,
آية رقم 12
ﯙﯚﯛ
ﯜ
«Ni Siku kubwa gani Mitume wameahirishiwa?»
آية رقم 13
ﯝﯞ
ﯟ
Wameahirishiwa Siku ya hukumu na uamuzi baina ya viumbe.
آية رقم 14
ﯠﯡﯢﯣﯤ
ﯥ
Na nilipi lililokujulisha wewe, ewe binadamu, ni siku gani hiyo ya kutolewa uamuzi na ni zipi shida zake na vituko vyake?
آية رقم 15
ﯦﯧﯨ
ﯩ
Maangamivu makubwa Siku hiyo ni ya wale waliyoikanusha Siku hii iliyoahidiwa.
آية رقم 16
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Kwani hatukuawaangamiza walitangulia kati ya umma waliopita kwa kuwakanusha kwao Mitume, kama vile watu wa Nūḥ, ‘Ād na Thamūd?
آية رقم 17
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Kisha tutawakutanisha na wao wale waliokuja nyuma kati ya wale waliokuwa ni kama wao katika ukanushaji na uasi.
آية رقم 18
ﯲﯳﯴ
ﯵ
Mfano wa uangamizaji huo mkali ndivyo tutakavyowafanya wahalifu kati ya makafiri wa Makkah, kwa kumkanusha kwao Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
آية رقم 19
ﯶﯷﯸ
ﯹ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa kila mwenye kuukanusha upweke wa Mwenyezi Mungu, unabii, kufufuliwa na kuhesabiwa.
آية رقم 20
ﭑﭒﭓﭔﭕ
ﭖ
Je kwani sisi hatukuwaumba nyinyi, enyi mkusanyiko wa makafiri, kutokana na maji dhaifu yaliyo matwevu nayo ni tone la manii,
آية رقم 21
ﭗﭘﭙﭚ
ﭛ
tukayaweka maji haya kwenye mahali palipohifadhika, napo ni kizazi cha mwanamke,
آية رقم 22
ﭜﭝﭞ
ﭟ
mpaka kipindi maalumu kinachojulikana na Mwenyezi Mungu Aliyetukuka?
آية رقم 23
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Tukaweza kumuumba, kumtia sura na kumtoa. Basi bora wa wenye kuweza ni s isi.
آية رقم 24
ﭤﭥﭦ
ﭧ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kukanusha uweza wetu.
آية رقم 25
ﭨﭩﭪﭫ
ﭬ
Je kwani hatukuifanya hii ardhi mnayoishi juu yake
آية رقم 26
ﭭﭮ
ﭯ
ikusanye juu ya mgongo wake walio hai wasiohesabika, na ndani ya matumbo yake wafu wasiodhibitika, na
آية رقم 27
tukajaalia iwe na majabali yaliyojikita yaliyo marefu ili isitikisike na nyinyi, na tukawanywesha maji tamu yaliyo mazuri?
آية رقم 28
ﭸﭹﭺ
ﭻ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa waliozikanusha neema hizi.
آية رقم 29
ﭼﭽﭾﭿﮀﮁ
ﮂ
Wataambiwa makafiri Siku ya Kiyama, «Endeni kwenye adhabu ya moto wa Jahanamu mliokuwa mkiukanusha duniani.
آية رقم 30
ﮃﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Endeni mjifinike kwenye kivuli cha moshi wa moto wa Jahanamu ambacho hapo panachembuka vipande vitatu.
آية رقم 31
ﮊﮋﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Kivuli hiko hakimfanyi mtu ahifadhike na joto la Siku hiyo wala hakizuii muwako wa Moto chochote.
آية رقم 32
ﮑﮒﮓﮔ
ﮕ
Hakika moto wa Jahanamu unarusha macheche makubwa ya moto, kila cheche moja katika hayo ni kama jengo lililoimarishwa katika ukubwa na urefu wa kuenda juu.
آية رقم 33
ﮖﮗﮘ
ﮙ
Kama kwamba hizo cheche za moto wa Jahanamu zinazopaa juu ni ngamia weusi ambao rangi yao imeingia kwenye umanjano.»
آية رقم 34
ﮚﮛﮜ
ﮝ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kukanusha mateso yaliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu.
آية رقم 35
ﮞﮟﮠﮡ
ﮢ
Hii ndiyo Siku ya Kiyama ambayo wakanushaji hawatatamka maneno ya kuwanufaisha
آية رقم 36
ﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
wala hawatapewa idhini ya kusema wakatoa nyudhuru, kwa kuwa hawatakuwa na udhuru wowote.
آية رقم 37
ﮨﮩﮪ
ﮫ
Maangamivu na adhabu kali kwa wenye kuikanusha siku hii na yaliyomo ndani yake.
آية رقم 38
ﮬﮭﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Hii ni Siku ambayo Mwenyezi Mungu Atatoa uamuzi baina ya viumbe, na ukweli na ubatilifu utapambanuka. Tutawakusanya nyinyi Siku hiyo, enyi makafiri wa ummah huu, pamoja na makafiri wa mwanzo miongoni mwa ummah waliopita.
آية رقم 39
ﯔﯕﯖﯗﯘ
ﯙ
Basi mkiwa na hila za kujitoa na adhabu, tumieni hila zenu na mziokoe nafsi zenu na msukosuko wa Mwenyezi Mungu na mateso Yake.
آية رقم 40
ﯚﯛﯜ
ﯝ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Kiyama.
آية رقم 41
ﯞﯟﯠﯡﯢ
ﯣ
Hakika ya wale waliomuogopa Mola wao duniani na wakaiogopa adhabu Yake kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake. Wao Siku ya Kiyama watakuwa kwenye vivuli vya miti vilivyonyoka, na chemchemi za maji zinazotembea,
آية رقم 42
ﯤﯥﯦ
ﯧ
na matunda mengi yanayopendwa na nafsi zao ambayo wao wanastarehe nayo. Hapo waambiwe,
آية رقم 43
ﯨﯩﯪﯫﯬﯭ
ﯮ
«Kuleni chakula chenye ladha na mnyweni kinywaji chenye kufurahisha kwa sababu ya matendo mema mliyoyatanguliza duniani.»
آية رقم 44
ﯯﯰﯱﯲ
ﯳ
Sisi, kwa mfano wa malipo hayo makubwa, tutawalipa watu wema katika matendo yao na utiifu wao kwetu.
آية رقم 45
ﯴﯵﯶ
ﯷ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya Malipo na Hesabu, na kuzikanusha sterehe na mateso yaliyomo Siku hiyo.
آية رقم 46
ﯸﯹﯺﯻﯼ
ﯽ
Kisha Mwenyezi Mungu Akawaonya makafiri kwa kusema, «Kuleni aina ya vyakula vya ladha duniani na stareheni kwa matamanio yake yenye kumalizika kwa muda mchache, hakika nyinyi ni wahalifu kwa kumshirikisha kwenu Mwenyezi Mungu.»
آية رقم 47
ﯾﯿﰀ
ﰁ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa.
آية رقم 48
ﰂﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
Na wanapoambiwa hawa washirikina, «Mswalieni Mwenyezi Mungu na mnyenyekeeni,» hawanyenyekei wala hawaswali, bali wanaendelea kuonyesha kiburi chao.
آية رقم 49
ﰉﰊﰋ
ﰌ
Maangamivu na adhabu kali Siku ya Kiyama kwa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu.
آية رقم 50
ﰍﰎﰏﰐ
ﰑ
Iwapo wao hawataiamini hii Qur’ani, basi wataamini kitabu gani na maneno gani baada yake? Na Qur’ani yenyewe ni Kitabu kilichobainisha kila kitu, kilicho wazi katika hekima zake, hukumu zake na habari zake, chenye kushinda katika matamko yake na maana yake.
تقدم القراءة