ترجمة معاني سورة الإنشقاق باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﭣﭤﭥ
ﭦ
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
آية رقم 2
ﭧﭨﭩ
ﭪ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
آية رقم 3
ﭫﭬﭭ
ﭮ
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
آية رقم 4
ﭯﭰﭱﭲ
ﭳ
Na milima yake kuvunjwa-vunjwa Siku hiyo.
آية رقم 5
ﭴﭵﭶ
ﭷ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
آية رقم 6
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
آية رقم 7
ﮁﮂﮃﮄﮅ
ﮆ
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
آية رقم 8
ﮇﮈﮉﮊ
ﮋ
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
آية رقم 9
ﮌﮍﮎﮏ
ﮐ
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
آية رقم 10
ﮑﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Na yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa nyuma ya mgongo wake,
آية رقم 11
ﮘﮙﮚ
ﮛ
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
آية رقم 12
ﮜﮝ
ﮞ
na ataingia Motoni.
آية رقم 13
ﮟﮠﮡﮢﮣ
ﮤ
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
آية رقم 14
ﮥﮦﮧﮨﮩ
ﮪ
Alidhani hatarudi kwa Muumba wake, akiwa hai, kwa kuhesabiwa.
آية رقم 15
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
آية رقم 16
ﯔﯕﯖ
ﯗ
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
آية رقم 17
ﯘﯙﯚ
ﯛ
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
آية رقم 18
ﯜﯝﯞ
ﯟ
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
آية رقم 19
ﯠﯡﯢﯣ
ﯤ
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti :kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
آية رقم 20
ﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
آية رقم 21
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
آية رقم 22
ﯲﯳﯴﯵ
ﯶ
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
آية رقم 23
ﯷﯸﯹﯺ
ﯻ
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
آية رقم 24
ﯼﯽﯾ
ﯿ
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
آية رقم 25
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
تقدم القراءة