سورة الإنشقاق

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة الإنشقاق باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
آية رقم 2
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
آية رقم 3
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
آية رقم 5
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
آية رقم 6
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
آية رقم 7
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
آية رقم 8
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
آية رقم 9
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
آية رقم 11
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
آية رقم 13
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
آية رقم 15
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
آية رقم 16
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
آية رقم 17
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
آية رقم 18
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
آية رقم 19
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti :kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
آية رقم 20
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
آية رقم 21
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
آية رقم 22
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
آية رقم 23
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
آية رقم 24
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
تقدم القراءة