ترجمة معاني سورة التكوير باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﭙﭚﭛ
ﭜ
Pindi jua litakapokunjwa, na mwangaza wake ukaondoka.
آية رقم 2
ﭝﭞﭟ
ﭠ
Na pindi nyota zitakapopuputika na nuru yake ikafutika.
آية رقم 3
ﭡﭢﭣ
ﭤ
Na pindi majabali yatakapoondoshawa kwenye uso wa ardhi yakawa ni vumbi linaloenea.
آية رقم 4
ﭥﭦﭧ
ﭨ
Na pindi ngamia wenye mimba watakapoachwa na kupuuzwa.
آية رقم 5
ﭩﭪﭫ
ﭬ
Na pindi wanyama mwitu watakapokusanywa na kutangamanishwa, ili Mwenyezi Mungu Awape nafasi ya kulipizana wao kwa wao.
آية رقم 6
ﭭﭮﭯ
ﭰ
Na pindi bahari zitakapowashwa moto zikawa ni moto unaowaka.
آية رقم 7
ﭱﭲﭳ
ﭴ
Na pindi nafsi zitakapokutanishwa na mfano wake na sampuli yake.
آية رقم 8
ﭵﭶﭷ
ﭸ
Na pindi mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa, Siku ya Kiyama, suala la kumbembeleza na kumkejeli aliyemzika:
آية رقم 9
ﭹﭺﭻ
ﭼ
ni kwa dhambi gani ilikuwa kuzikwa kwake?
آية رقم 10
ﭽﭾﭿ
ﮀ
Na pindi kurasa za matendo zitakapoonyeshwa.
آية رقم 11
ﮁﮂﮃ
ﮄ
Na pindi mbingu zitakapong’olewa na kuondoshwa zilipokuwa.
آية رقم 12
ﮅﮆﮇ
ﮈ
Na pindi Moto utakapowashwa na ukawaka.
آية رقم 13
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Na pindi Pepo , Nyumba ya Neema, itakaposongezewa watu wake wachamungu.
آية رقم 14
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Litakapotokea hilo, itayakinisha kila nafsi na kujua kile ilichokitanguliza cha kheri au shari.
آية رقم 15
ﮒﮓﮔ
ﮕ
Anaapa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa nyota zinazofichika nuru yake mchana,
آية رقم 16
ﮖﮗ
ﮘ
zinazotembea na zinazoghibu katika anga zake.
آية رقم 17
ﮙﮚﮛ
ﮜ
Na Anaapa kwa usiku unapojitokeza na giza lake.
آية رقم 18
ﮝﮞﮟ
ﮠ
Na kwa asubuhi unapojitokeza mwangaza wake.
آية رقم 19
ﮡﮢﮣﮤ
ﮥ
Hakika Qur’ani ni ujumbe wa mjumbe mtukufu , naye ni Jibrili, amani imshukike.
آية رقم 20
ﮦﮧﮨﮩﮪﮫ
ﮬ
Mwenye nguvu katika kuyapitisha yale anayoamrishwa. Mwenye cheo cha juu kwa Mwenyezi Mungu. Anayesikilizwa na Malaika.
آية رقم 21
ﮭﮮﮯ
ﮰ
Anayeaminiwa juu ya Wahyi anaoteremka nao.
آية رقم 22
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Hakuwa Muhammad mnayemjua ni mwendawazimu.
آية رقم 23
ﯖﯗﯘﯙ
ﯚ
Na kwa hakika Muhammad alimuona Jibrili anayemjia na utume katika pambizo kubwa.
آية رقم 24
ﯛﯜﯝﯞﯟ
ﯠ
Wala yeye hafanyi ubakhili katika kufikisha Wahyi.
آية رقم 25
ﯡﯢﯣﯤﯥ
ﯦ
Wala haikuwa hii Qur’ani ni neno la Shetani aliyefukuzwa na kutolewa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu. Lakini Qur’ani hii ni maneno ya Mwenyezi Mungu na ni Wahyi wake.
آية رقم 26
ﯧﯨ
ﯩ
Akili zenu zawapeleka wapi katika kukanusha baada ya hoja hizi zilizo wazi na zenye nguvu?
آية رقم 27
ﯪﯫﯬﯭﯮ
ﯯ
Hayakuwa haya isipokuwa ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu yanapewa watu wote.
آية رقم 28
ﯰﯱﯲﯳﯴ
ﯵ
Kwa atakaye, kati yenu, kulingana juu ya haki na Imani.
آية رقم 29
Wala nyinyi hamtotaka isipokuwa kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote.
تقدم القراءة