ترجمة معاني سورة المعارج باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Ameapiza mwenye kuapiza miongoni mwa washirikina, kujiapiza mwenyewe na kuwaapiza watu wake kuteremkiwa na adhabu,
آية رقم 2
ﯔﯕﯖﯗ
ﯘ
nayo ni yenye kuwashukia bila shaka Siku ya Kiyama.
آية رقم 3
ﯙﯚﯛﯜ
ﯝ
Hakuna mzuiaji yoyote wa kuizuia isipokuwa Mwenyezi Mungu, Mwenye utukufu na haiba.
آية رقم 4
Malaika na Jibrili wanapanda kuenda Kwake, Aliyetukuka, kwa siku moja ambayo kadiri yake ni myaka elfu hamsini katika myaka ya duniani, nayo kwa aliyeamini ni kama muda wa Swala moja ya faradhi.
آية رقم 5
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Basi vumilia, ewe Mtume, kule kufanya kwao shere na kutaka kwao wafikiwe na adhabu kwa haraka, uvumilivu usiokuwa na babaiko wala kumshtakia asiyekuwa Mwenyezi Mungu.
آية رقم 6
ﯮﯯﯰ
ﯱ
Kwa kweli makafiri wanaiona adhabu kuwa iko mbali na wanaona kuwa si yenye kutukia.
آية رقم 7
ﯲﯳ
ﯴ
Na sisi tunaiona ni yenye kutukia kwa kipindi cha karibu bila shaka.
آية رقم 8
ﯵﯶﯷﯸ
ﯹ
Siku ambayo mbingu itayayuka iwe ni kama rojo la mafuta,
آية رقم 9
ﯺﯻﯼ
ﯽ
na majabali yawe ni kama sufi iliyochanganywa na iliyoshanuliwa na kupeperushwa na upepo.
آية رقم 10
ﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Wala mtu hatamuuliza jamaa yake wa karibu kuhusu jambo lake, kwani kila mmoja ameshughulishwa na nafsi yake.
آية رقم 11
Watawaona na watawajua, na hakuna yoyote atakayeweza kumnufaisha yoyote. Kafiri atatamani lau ajikomboa nafsi yake na adhabu ya Siku ya Kiyama kwa watoto wake,
آية رقم 12
ﭜﭝ
ﭞ
mkewe, nduguye,
آية رقم 13
ﭟﭠﭡ
ﭢ
jamaa zake wanaomuhami na ambao anajinasibisha nao kwa ujamaa
آية رقم 14
ﭣﭤﭥﭦﭧﭨ
ﭩ
na kwa wote walio kwenye ardhi miongoni mwa binadamu na wengineo ili aokoke na adhabu ya Mwenyezi Mungu.
آية رقم 15
ﭪﭫﭬﭭ
ﭮ
Mambo siyo kama vile unavyotamani yawe, ewe kafiri, ya kujikomboa.
آية رقم 16
ﭯﭰ
ﭱ
Huo ni moto wa Jahanamu, moto wake unawaka na kuroroma, joto lake linatoa kwa nguvu ngozi ya kichwa na sehemu nyingine za mwili,
آية رقم 17
ﭲﭳﭴﭵ
ﭶ
unamwita aliyeipa mgongo haki duniani na akaacha kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake,
آية رقم 18
ﭷﭸ
ﭹ
na akakusanya mali na kuyaweka kwenye mahazina yake na asitekeleze amri ya Mwenyezi Mungu kwenye mali hayo.
آية رقم 19
ﭺﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Hakika binadamu ameumbwa akiwa na tabia ya babaiko na pupa.
آية رقم 20
ﮀﮁﮂﮃ
ﮄ
Yakimpata makero na shida, anababaika sana na kufa moyo.
آية رقم 21
ﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na yakimpata mambo mazuri na ukunjufu wa maisha, huwa ni mwingi wa kuzuia na.
آية رقم 22
ﮊﮋ
ﮌ
Isipokuwa wenye kusimamisha Swala,
آية رقم 23
ﮍﮎﮏﮐﮑ
ﮒ
wanaochunga kuitekeleza katika nyakati zake zote, hakuna shughuli yoyote inayowashughulisha nayo.
آية رقم 24
ﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Na wale ambao katika mali yao kuna fungu maalumu alililowafaradhia Mwenyezi Mungu, nalo ni Zaka
آية رقم 25
ﮙﮚ
ﮛ
wanaozitoa kwa anayeomba msaada na kwa na kwa asiyeomba.
آية رقم 26
ﮜﮝﮞﮟ
ﮠ
Na wale ambao wanaiamini Siku ya kuhesabiwa na kulipwa wakajiandaa nayo kwa matendo mema.
آية رقم 27
ﮡﮢﮣﮤﮥﮦ
ﮧ
Na wale ambao wao wanaiogopa adhabu ya Mwenyezi Mungu,
آية رقم 28
ﮨﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
kwani adhabu ya Mola wao haipaswi kwa yoyote kujiaminisha nayo.
آية رقم 29
ﮮﮯﮰﮱ
ﯓ
Na wale ambao wao ni wenye kutunza tupu zao na kila alichokiharamishia Mwenyezi Mungu,
آية رقم 30
isipokuwa wake zao na vijakazi vyao, hakika wao kwa hao hawapatilizwi.
آية رقم 31
Basi mwenye kutaka kumaliza matamanio yake ya kimwili kwa wasiokuwa wake zake au vijakazi vyake, basi hao ndio wenye kukiuka mipaka ya halali kuingia kwenye haramu.
آية رقم 32
ﯧﯨﯩﯪﯫ
ﯬ
Na wale ambao wanazitunza amana za Mwenyezi Mungu na amana za waja, na wanatunza ahadi zao pamoja na Mwenyezi Munmgu, Aliyetukuka, na pamoja na waja.
آية رقم 33
ﯭﯮﯯﯰ
ﯱ
Na wale ambao wanatekeleza ushahidi wao kwa ukweli bila kubadilisha au kuficha.
آية رقم 34
ﯲﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na wale ambao wanatunza utekelezaji Swala wala hawaharibu chochote cha wajibu katika hiyo Swala.
آية رقم 35
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Hao waliosifika kwa sifa hizo njema, ni wenye kutulia kwenye mabustani ya Pepo ya starehe, ni wenye kukirimiwa humo kwa kila aina ya takrima.
آية رقم 36
ﯽﯾﯿﰀﰁ
ﰂ
Ni msukumo gani unaowasukuma makafiri watembee kwa haraka kuelekea upande wako, ewe Mtume, na huku wamenyosha shingo zao kwako, wamekukabili kwa macho yao,
آية رقم 37
ﰃﰄﰅﰆﰇ
ﰈ
wanajikusanya kuliani kwako na kushotoni kwako, wakiwa wamekaa kwa kupiga maduara na wamejigawa vikundi mbalimbali, wanazungumza na kuona ajabu?
آية رقم 38
Je ana tamaa kila mmoja miongoni mwa makafiri kuwa Mwenyezi Mungui Atamuingiza kwenye Pepo ya starehe ya daima? Mambo siyo kama vile wanavyotazamia. Wao hawataiingia hiyo Pepo kabisa.
آية رقم 39
ﰒﰓﰔﰕﰖﰗ
ﰘ
Hakika sisi tumewaumba kwa kile wanachokijua cha maji matwevu kama wengineo, na vilevile hawakuamini. Basi vipi watapata heshima ya kuingia Pepo ya sterehe?
آية رقم 40
Sivyo hivyo. Najiapia Mimi Mwenyewe niliye Mola wa pande za kuchomoza na kutua jua, mwezi na sayari nyinginezo, kwa yanayopatikana humo miongoni mwa dalili waziwazi za kujulisha kufufuliwa,
آية رقم 41
kuwa Sisi tunaweza kuwaleta watu badala yao walio bora zaidi kuliko wao na watiifu zaidi wa Mwenyezi Mungu. Na hakuna yoyote atakayetushinda na kutuponyoka na kutuelemea iwapo tunataka kumrudisha uhai baada ya kufa.
آية رقم 42
Basi waache wavame kwenye ubatilifu wao na wacheze kwenye ulimwengu wao mpaka wakutane na Siku ya Kiyama ambayo wanaahidiwa kuwa wataadhibiwa.
آية رقم 43
Siku watakapotoka makaburini wakienda kwa haraka, kama wlivyokuwa duniani wakienda mbio na haraka kwa waungu wao wakiwaabudu badala ya Mwenyezi Mungu,
آية رقم 44
hali ya kuwa macho yao ni madhalilifu yanatazama chini, wamefinikwa na unyonge na utwevu. Hiyo ndiyo Siku waliyoahidiwa duniani na walikuwa wakiifanyia shere na kuikanusha.
تقدم القراءة