سورة الليل

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة الليل باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa usiku unapoifinika ardhi na vilivyoko juu yake kwa giza lake.
آية رقم 2
Na kwa mchana unapofunuka mwangaza wake kutoka kwenye giza la usiku.
آية رقم 4
Kuwa vitendo vyenu vinatofautiana: kuna wenye kufanyia dunia na wenye kufanyia Akhera.
آية رقم 5
Ama mwenye kutoa kwenye mali yake, akamcha Mwenyezi Mungu katika huko kutoa,
آية رقم 6
akaamini «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na Imani hiyo na akaamini malipo yanayofungamana nayo,
آية رقم 7
Tutamuongoza na kumuafikia njia za kheri na wema na kumsahilishia mambo yake.
آية رقم 8
Na ama mwenye kuyafanyia ubakhili mali yake, asiwe na haja ya malipo ya Mola wake,
آية رقم 9
akakanusha neno la «Lā Ilāha Illā Allāh» na yanayotakiwa na neno hilo na akakanusha malipo yanayofungamana nalo,
آية رقم 10
Tutamnyoshea njia za mateso.
آية رقم 11
Wala hayatamfaa yeye mali yake aliyoyafanyia ubakhili atakapotumbukia Motoni.
آية رقم 12
Ni juu Yetu, kwa fadhila Zetu na busara Yetu, kueleza njia ya uongofu yenye kufikisha kwa Mwenyezi Mungu na ya upotevu.
آية رقم 13
Na Sisi Tuna mamlaka ya maisha ya Akhera na maisha ya ulimwenguni.
آية رقم 14
Ndipo nikawaonya , enyi watu, na kuwatisha moto wenye kuwaka, nao ni moto wa Jahanamu.
آية رقم 15
Hataingia Moto huo isipokuwa aliyekuwa mbaya sana. Mwenye kumkanusha Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie,
آية رقم 16
na akakataa kumwamini na kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake.
آية رقم 17
Na ataepushwa nao mchaji Mwenyezi Mungu sana.
آية رقم 18
Ambaye hutoa mali yake kwa kutaka nyongeza za kheri
آية رقم 20
Lakini anatoa kwa kutaka uso wa Mola wake na radhi zake. Basi Mwenyezi Mungu atampa,
آية رقم 21
huko Peponi, malipo ya kumridhisha.
تقدم القراءة