ترجمة معاني سورة الغاشية باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﭽﭾﭿﮀ
ﮁ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
آية رقم 2
ﮂﮃﮄ
ﮅ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
آية رقم 3
ﮆﮇ
ﮈ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
آية رقم 4
ﮉﮊﮋ
ﮌ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
آية رقم 5
ﮍﮎﮏﮐ
ﮑ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
آية رقم 6
ﮒﮓﮔﮕﮖﮗ
ﮘ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
آية رقم 7
ﮙﮚﮛﮜﮝﮞ
ﮟ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
آية رقم 8
ﮠﮡﮢ
ﮣ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
آية رقم 9
ﮤﮥ
ﮦ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
آية رقم 10
ﮧﮨﮩ
ﮪ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
آية رقم 11
ﮫﮬﮭﮮ
ﮯ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
آية رقم 12
ﮰﮱﯓ
ﯔ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
آية رقم 13
ﯕﯖﯗ
ﯘ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
آية رقم 14
ﯙﯚ
ﯛ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
آية رقم 15
ﯜﯝ
ﯞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
آية رقم 16
ﯟﯠ
ﯡ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
آية رقم 17
ﯢﯣﯤﯥﯦﯧ
ﯨ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
آية رقم 18
ﯩﯪﯫﯬ
ﯭ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
آية رقم 19
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
آية رقم 20
ﯳﯴﯵﯶ
ﯷ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
آية رقم 21
ﯸﯹﯺﯻ
ﯼ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
آية رقم 22
ﯽﯾﯿ
ﰀ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
آية رقم 23
ﭑﭒﭓﭔ
ﭕ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
آية رقم 24
ﭖﭗﭘﭙ
ﭚ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
آية رقم 25
ﭛﭜﭝ
ﭞ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
آية رقم 26
ﭟﭠﭡﭢ
ﭣ
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
تقدم القراءة