سورة الغاشية

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

ترجمة معاني سورة الغاشية باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس

آية رقم 1
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
آية رقم 2
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
آية رقم 3
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
آية رقم 4
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
آية رقم 6
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
آية رقم 7
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
آية رقم 8
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
آية رقم 9
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
آية رقم 10
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
آية رقم 12
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
آية رقم 14
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
آية رقم 15
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
آية رقم 16
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
آية رقم 17
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
آية رقم 18
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
آية رقم 19
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
آية رقم 21
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
آية رقم 22
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
آية رقم 23
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
آية رقم 25
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
تقدم القراءة