ترجمة معاني سورة النبأ باللغة السواحلية من كتاب الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس
آية رقم 1
ﭑﭒ
ﭓ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
آية رقم 2
ﭔﭕﭖ
ﭗ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
آية رقم 3
ﭘﭙﭚﭛ
ﭜ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
آية رقم 4
ﭝﭞ
ﭟ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
آية رقم 5
ﭠﭡﭢ
ﭣ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
آية رقم 6
ﭤﭥﭦﭧ
ﭨ
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
آية رقم 7
ﭩﭪ
ﭫ
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
آية رقم 8
ﭬﭭ
ﭮ
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
آية رقم 9
ﭯﭰﭱ
ﭲ
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
آية رقم 10
ﭳﭴﭵ
ﭶ
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
آية رقم 11
ﭷﭸﭹ
ﭺ
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
آية رقم 12
ﭻﭼﭽﭾ
ﭿ
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
آية رقم 13
ﮀﮁﮂ
ﮃ
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
آية رقم 14
ﮄﮅﮆﮇﮈ
ﮉ
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
آية رقم 15
ﮊﮋﮌﮍ
ﮎ
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
آية رقم 16
ﮏﮐ
ﮑ
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
آية رقم 17
ﮒﮓﮔﮕﮖ
ﮗ
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
آية رقم 18
ﮘﮙﮚﮛﮜﮝ
ﮞ
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
آية رقم 19
ﮟﮠﮡﮢ
ﮣ
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
آية رقم 20
ﮤﮥﮦﮧ
ﮨ
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
آية رقم 21
ﮩﮪﮫﮬ
ﮭ
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
آية رقم 22
ﮮﮯ
ﮰ
Kwa makafiri ndio marejeo.
آية رقم 23
ﮱﯓﯔ
ﯕ
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
آية رقم 24
ﯖﯗﯘﯙﯚﯛ
ﯜ
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
آية رقم 25
ﯝﯞﯟ
ﯠ
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
آية رقم 26
ﯡﯢ
ﯣ
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
آية رقم 27
ﯤﯥﯦﯧﯨ
ﯩ
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
آية رقم 28
ﯪﯫﯬ
ﯭ
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
آية رقم 29
ﯮﯯﯰﯱ
ﯲ
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
آية رقم 30
ﯳﯴﯵﯶﯷ
ﯸ
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
آية رقم 31
ﭑﭒﭓ
ﭔ
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
آية رقم 32
ﭕﭖ
ﭗ
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
آية رقم 33
ﭘﭙ
ﭚ
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
آية رقم 34
ﭛﭜ
ﭝ
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
آية رقم 35
ﭞﭟﭠﭡﭢﭣ
ﭤ
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
آية رقم 36
ﭥﭦﭧﭨﭩ
ﭪ
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
آية رقم 37
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
آية رقم 38
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
آية رقم 39
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
آية رقم 40
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
تقدم القراءة