وَلَوۡ أَنَّهُمۡ صَبَرُواْ حَتَّىٰ تَخۡرُجَ إِلَيۡهِمۡ لَكَانَ خَيۡرٗا لَّهُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na lau wao wangeli ngojea mpaka uwatokee ingeli kuwa kheri kwao. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye maghfira, Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau wangalisubiri mpaka ukawatokea ingalikuwa bora zaidi kwao mbele ya Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu Amewaamrisha wao kukuheshimu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha kwa yale yaliyotokea kwao ya madhambi na utovu wa adabu kwa kutojua kwao, ni Mwingi wa rehema kwao kwa kutowaharakishia mateso.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس