فَذَاقَتۡ وَبَالَ أَمۡرِهَا وَكَانَ عَٰقِبَةُ أَمۡرِهَا خُسۡرًا
Basi ikauonja ubaya wa mambo yake; na mwisho wa mambo yao ilikuwa khasara.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
tukawahesabu juu ya matendo yao duniani hesabu kali mno na tukawaadhibu adhabu kubwa na mbaya, wakauonja mwisho mbaya wa ujeuri wao na ukafiri wao, na mwisho wa ukafiri wao ulikuwa ni maangamivu na hasara, hapana hasara nyingine baada ya hiyo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس