وَمَن لَّا يُجِبۡ دَاعِيَ ٱللَّهِ فَلَيۡسَ بِمُعۡجِزٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَيۡسَ لَهُۥ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءُۚ أُوْلَـٰٓئِكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Na wasio mwitikia Mwitaji wa Mwenyezi Mungu basi hao hawatashinda katika ardhi, wala hawatakuwa na walinzi mbele yake. Hao wamo katika upotovu ulio dhaahiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na asiyemuitikia Mtume wa Mwenyezi Mungu katika yale aliyoyalingania, basi yeye hatamshinda Mwenyezi Mungu katika ardhi Akitaka kumuadhibu, wala hatakuwa na wasaidizi badala ya Mwenyezi Mungu, wenye kumkinga na adhabu Yake. Hao watakuwa wametoka nje ya haki waziwazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس