يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَكُمۡ تَفَسَّحُواْ فِي ٱلۡمَجَٰلِسِ فَٱفۡسَحُواْ يَفۡسَحِ ٱللَّهُ لَكُمۡۖ وَإِذَا قِيلَ ٱنشُزُواْ فَٱنشُزُواْ يَرۡفَعِ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنكُمۡ وَٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ دَرَجَٰتٖۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Enyi mlio amini! Mkiambiwa: Fanyeni nafasi katika mabaraza, basi fanyeni nafasi. Na Mwenyezi Mungu atakufanyieni nyinyi nafasi. Na mkiambiwa: Ondokeni, basi ondokeni. Mwenyezi Mungu atawainua walio amini miongoni mwenu, na walio pewa ilimu daraja za juu. Na Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayo yatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Mkitakiwa mpanane nafasi kwenye mabaraza basi peaneni nafasi, na mkifanya hivyo Mwenyezi Mungu Atawakunjulia nafasi duniani na Akhera. Na mkitakiwa kwenu, enyi Waumini, muinuke katika mabaraza yenu kwa jambo lolote lenye kheri kwenu, basi inukeni. Mwenyezi Mungu Anavipandisha vyeo vya Waumini miongoni mwenu, na Anavipandisha vyeo vya wenye elimu daraja nyingi kwa kuwapatia malipo mema na daraja za kupata radhi. Na Mwenyezi Mungu Anayatambua matendo yenu, hakuna chochote kinachofichamana Kwake katika hayo, na Yeye ni mwenye kuwalipa nyinyi kwayo. Katika aya pana kutukuza cheo cha wanavyuoni na utukufu wao na kutukuzwa daraja zao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس