يَوۡمَ يَبۡعَثُهُمُ ٱللَّهُ جَمِيعٗا فَيَحۡلِفُونَ لَهُۥ كَمَا يَحۡلِفُونَ لَكُمۡ وَيَحۡسَبُونَ أَنَّهُمۡ عَلَىٰ شَيۡءٍۚ أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡكَٰذِبُونَ
Siku atakayo wafufua Mwenyezi Mungu wote, wamuwapie kama wanavyo kuwapieni nyinyi. Na watadhani kuwa wamepata kitu! Kwa hakika hao ndio waongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Siku ya Kiyama, Mwenyezi Mungu Atawafufua wanafiki wote kutoka makaburini mwao wakiwa hai, na hapo wamuapie Yeye kuwa wao walikuwa Waumini kama walivyokuwa wakiwaapia nyinyi, enyi Waumini, duniani. Na watadhani kuwa hilo litawanufaisha kwa Mwenyezi Mungu kama lilivyokuwa linawanufaisha ulimwenguni kwa Waislamu. Basi jua na utanabahi kuwa wao ndio waliofikia upeo katika urongo ambao hawakuufikia wasiokuwa wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس