ٱلَّذِينَ يُظَٰهِرُونَ مِنكُم مِّن نِّسَآئِهِم مَّا هُنَّ أُمَّهَٰتِهِمۡۖ إِنۡ أُمَّهَٰتُهُمۡ إِلَّا ٱلَّـٰٓـِٔي وَلَدۡنَهُمۡۚ وَإِنَّهُمۡ لَيَقُولُونَ مُنكَرٗا مِّنَ ٱلۡقَوۡلِ وَزُورٗاۚ وَإِنَّ ٱللَّهَ لَعَفُوٌّ غَفُورٞ
Wale miongoni mwenu wanao watenga wake zao, hao si mama zao. Hawakuwa mama zao ila wale walio wazaa. Na hakika hao wanasema neno linalo chusha, na la uwongo. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kughufiria, Mwenye kusamehe.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
wale wanaowafananisha wake zao na mama zao, kwa kutoka mwanamume miongoni mwao kumwambia mkewe, «Wewe kwangu ni kama mgongo ya mamangu» yaani kuwa kumuingilia ni haramu, wamemuasi Mwenyezi Mungu na wameenda kinyume na Sheria. Na wake zao si mama zao kihakika, bali wao ni wake zao; mama zao ni wale tu waliowazaa wao. Na hawa wanaowafananisha wake zao na mama zao, kwa hakika, wanasema neno la urongo lililo baya lisilo sahihi. Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa kusamahe na kusitiri kwa wale ambao yametokea kwao baadhi ya mambo ya uvunjaji Sheria kisha wakayarakebisha kwa kutubia kidhati.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس