يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَنَٰجَيۡتُمۡ فَلَا تَتَنَٰجَوۡاْ بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَمَعۡصِيَتِ ٱلرَّسُولِ وَتَنَٰجَوۡاْ بِٱلۡبِرِّ وَٱلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ
Enyi mlio amini! Mnapo nong'ona msinong'one kwa sababu ya mambo ya madhambi, na uadui, na kumuasi Mtume. Bali nong'onezane kwa kutenda mema na kuacha maovu. Na mcheni Mwenyezi Mungu ambaye kwake mtakusanywa nyote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Mnapozungumza baina yenu kwa siri, msizungumze maneno ya dhambi au yenye uadui kwa wengine msiokuwa nyinyi au yanayoenda kinyume na amri ya Mtume. Na zungumzeni yale yenye kheri, utiifu na wema, na muogopeni Mwenyezi Mungu kwa kufuata amri Zake na kujiepusha na makatazo Yake, Kwani Kwake Yeye Peke Yake ndipo mtakaporudi na matendo yenu yote na maneno yenu Aliyowadhibitia, na Atawalipa kwayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس