Al-Hashr
سَبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۖ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ
Vinamsabihi, Vinamtakasa Mwenyezi Mungu viliomo katika mbingu na viliomo katika ardhi. Naye ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Vimemtakasa Mwenyezi Mungu na kumuepusha na kila kisichonasibiana na Yeye, vilivyoko mbinguni na vilivyoko ardhini, na Yeye Ndiye Mshindi Asiyekuwa na mwenye kushindana na Yeye, Mwingi wa hekima katika makadirio Yake, uendeshaji Wake na utengezaji Wake na Sheria Zake, Anaweka kila jambo mahali pake panapostahiki.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس