لَئِنۡ أُخۡرِجُواْ لَا يَخۡرُجُونَ مَعَهُمۡ وَلَئِن قُوتِلُواْ لَا يَنصُرُونَهُمۡ وَلَئِن نَّصَرُوهُمۡ لَيُوَلُّنَّ ٱلۡأَدۡبَٰرَ ثُمَّ لَا يُنصَرُونَ
Pindi wakitolewa hawatatoka pamoja nao, na wakipigwa vita hawatawasaidia. Na kama wakiwasaidia basi watageuza migongo; kisha hawatanusuriwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Lau Mayahudi watatolewa Madina, wanafiki hawatatoka pamoja na wao, na lau watapigwa vita hawatapigana pamoja na wao kama walivyoahidi. Na lau watapigana pamoja na wao wangalipa mgongo hali ya kukimbia kwa kushindwa, kisha Mwenyezi Mungu Hatawanusuru, bali Atawaacha bila kuwasaidia na Atawadhalilisha.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس