هُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ رَسُولَهُۥ بِٱلۡهُدَىٰ وَدِينِ ٱلۡحَقِّ لِيُظۡهِرَهُۥ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُشۡرِكُونَ
Yeye ndiye aliye mtuma Mtume wake kwa uwongofu na Dini ya haki ili ipate kuzishinda dini zote, ijapo kuwa washirikina watachukia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Yeye Ndiye Aliyemtumiliza Mtume Wake Muhammad kwa Qur’ani na Dini ya haki ili Aifanye kuwa juu ya dini zilizo kinyume nayo japokuwa washirikina watachukia hilo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس