وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ خَٰلِدِينَ فِيهَاۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Na walio kufuru na wakakadhibisha Ishara zetu, hao ni watu wa Motoni, watadumu humo milele. Na hayo ndiyo marudio mabaya.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale ambao wanapinga kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Mola wa haki na wakazikanusha dalili za kuwa Yeye Ndiye Mola na hoja za uungu Wake Alizowatuma nazo Mitume Wake, hao ni watu wa Motoni, ni wenye kukaa humo milele. Moto huo wa Jahanamu ni marejeo maovu mno watakayofikia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس