يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَيَعۡلَمُ مَا تُسِرُّونَ وَمَا تُعۡلِنُونَۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Anajua viliomo katika mbingu na ardhi, na anajua mnayo yaficha na mnayo yatangaza. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliomo vifuani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Anajua, kutakasika na kutukuka ni Kwake, kila kilichoko mbinguni na ardhini, na Anakijua mnachokificha, enyi watu, na mnachokidhihirisha. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yale yanayodhamiriawa na vifua na kufichwa na nafsi
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس