أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَبَؤُاْ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَبۡلُ فَذَاقُواْ وَبَالَ أَمۡرِهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Kwani haikukujieni khabari ya walio kufuru kabla, wakaonja matokeo mabaya ya mambo yao? Na wao wana adhabu iliyo chungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Je haikuwajia nyinyi, enyi washirikina, habari ya wale waliokufuru miongoni mwa watu waliopita kabla yenu, ulipowafikia wao mwisho mbaya wa ukafiri wao na uovu wa vitendo vyao hapa ulimwenguni na kuwa wao kesho Akhera watakuwa na adhabu kali iumizayo?
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس