أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدٗاۖ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ يَـٰٓأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۚ قَدۡ أَنزَلَ ٱللَّهُ إِلَيۡكُمۡ ذِكۡرٗا
Mwenyezi Mungu aliwaandalia adhabu kali. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, enyi wenye akili, mlio amini! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteremshieni Ukumbusho,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Amewaandalia watu hawa, waliokiuka mipaka na wakaenda kinyume na amri za Mwenyezi Mungu na amri za Mitume Wake, adhabu kali sana. Basi muogopeni Mwenyezi Mungu na mjihadhari na mambo Anayoyachukia, enyi watu wenye akili zilizokomaa, mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mitume Wake na mkazifuata Sheria Zake kivitendo! Kwa hakika Mwenyezi Mungu Ameteremsha kwenu, enyi Waumini, Ukumbusho wa kuwakumbusha nao na kuwazindusha juu ya fungu lenu la kumuamini Mwenyezi Mungu na kuwa watiifu Kwake kivitendo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس