وَمَرۡيَمَ ٱبۡنَتَ عِمۡرَٰنَ ٱلَّتِيٓ أَحۡصَنَتۡ فَرۡجَهَا فَنَفَخۡنَا فِيهِ مِن رُّوحِنَا وَصَدَّقَتۡ بِكَلِمَٰتِ رَبِّهَا وَكُتُبِهِۦ وَكَانَتۡ مِنَ ٱلۡقَٰنِتِينَ
Na Mariamu binti wa Imrani, aliye linda ubikira wake, na tukampulizia humo kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi na Vitabu vyake, na alikuwa miongoni mwa wat'iifu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Anapiga mfano kwa walioamini. Mfano wenyewe ni Maryam binti 'Imran aliyeihifadhi tupu yake na akailinda na uzinifu, basi mwenyezi Mungu Akamuamrisha Jibrili, amani imshukie, apulize kwenye mfuko wa nguo yake. Na ule mpulizo ukafika kwenye uzao wake. Hapo akabeba mimba ya ‘Īsā, amani imshukie, akayaamini maneno ya Mola wake, akafuata kivitendo Sheria Zake Alizozipasisha kwa waja Wake na vitabu Vyake Alivyoviteremsha kwa Mitume Wake, na akawa ni miongoni mwa wale wenye kumtii Yeye.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس