مَن كَانَ يُرِيدُ ٱلۡعِزَّةَ فَلِلَّهِ ٱلۡعِزَّةُ جَمِيعًاۚ إِلَيۡهِ يَصۡعَدُ ٱلۡكَلِمُ ٱلطَّيِّبُ وَٱلۡعَمَلُ ٱلصَّـٰلِحُ يَرۡفَعُهُۥۚ وَٱلَّذِينَ يَمۡكُرُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ لَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدٞۖ وَمَكۡرُ أُوْلَـٰٓئِكَ هُوَ يَبُورُ
Mwenye kutaka utukufu basi utukufu wote uko kwa Mwenyezi Mungu. Kwake Yeye hupanda neno zuri, na a'mali njema Yeye huitukuza. Na wanao panga vitimbi vya maovu watapata adhabu kali. Na vitimbi vya hao vitaondokea patupu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Yoyote yule atakaye enzi ya duniani au Akhera, basi aitake kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na hilo halipatikani isipokuwa kwa kumtii Yeye, kwani enzi yote ni ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kujienzi na kiumbe, Mwenyezi Mungu Atamdhalilisha; na Mwenye kujienzi na Muumba, Mwenyezi Mungu Atamtukuza. Kwake Yeye utajo wake utapanda, na tendo lema Analiinua juu. Na wale wenye kutenda mabaya watapewa adhabu kali. Na vitimbi vya hao vitaangamia na vitaharibika na havitawafaidisha kitu chochote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس