لِيُوَفِّيَهُمۡ أُجُورَهُمۡ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضۡلِهِۦٓۚ إِنَّهُۥ غَفُورٞ شَكُورٞ
Ili Yeye awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na awazidishie kutokana na fadhila zake. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe Mwenye shukrani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ili Awatimizie Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, malipo mema ya matendo yao yakiwa kamili bila kupunguzwa, na wataongezewa mema kwa fadhila Zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Msamehefu sana wa makosa yao, ni Mwingi wa shukrani kwa mema yao, Atawalipa kwa mema hayo malipo mazuri mengi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس