جَنَّـٰتُ عَدۡنٖ يَدۡخُلُونَهَا يُحَلَّوۡنَ فِيهَا مِنۡ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٖ وَلُؤۡلُؤٗاۖ وَلِبَاسُهُمۡ فِيهَا حَرِيرٞ
Mabustani ya milele watayaingia. Huko watavikwa vikuku vya dhahabu, na lulu, na nguo zao humo ni za hariri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Pepo za makazi ya daima kwa wale ambao Mwenyezi Mungu Amewarithisha Kitabu Chake, watapambwa huko kwa vikuku vya dhahabu na kwa lulu. Na mavazi yao ya kawaida huko Peponi ni hariri, yaani: nguo laini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس