وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَهُمۡ نَارُ جَهَنَّمَ لَا يُقۡضَىٰ عَلَيۡهِمۡ فَيَمُوتُواْ وَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُم مِّنۡ عَذَابِهَاۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي كُلَّ كَفُورٖ
Na walio kufuru watakuwa na Moto wa Jahannamu, hawahukumiwi wakafa, wala hawatapunguziwa adhabu yake. Hivyo ndivyo tunavyo mlipa kila mwenye kuzidi ukafiri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, watakuwa na Moto wa Jahanamu uliowashwa. Hakutatolewa uamuzi juu yao kuwa wafe wakapata kufa na kupumzika, wala hawatapunguziwa adhabu yake. Mfano wa malipo hayo, Mwenyezi Mungu Anamlipa kila mwenye kuendelea kwenye ukafiri na kuwa na ukakamavu juu yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس