إِنَّ ٱللَّهَ عَٰلِمُ غَيۡبِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّهُۥ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ
Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa siri za mbinguni na ardhi. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliomo vifuani.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwa hakika Mwenyezi Mungu Anakiona kila kisichoonekana mbinguni na ardhini, na kwa hakika Yeye ni Mjuzi mno wa vilivyofichamana nyoyoni. Basi muogopeni Asiwaone mkiwa mko katika hali ya kudhamiria shaka au ushirikina katika kumpwekeshaYeye au juu ya unabii wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani ziwashukie, au muende kinyume na amri Yake katika mambo madogo ya hayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس