قُلۡ مَا كُنتُ بِدۡعٗا مِّنَ ٱلرُّسُلِ وَمَآ أَدۡرِي مَا يُفۡعَلُ بِي وَلَا بِكُمۡۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّ وَمَآ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Sema: Mimi si kiroja miongoni mwa Mitume. Wala sijui nitakavyo fanywa wala nyinyi. Mimi nafuata niliyo funuliwa tu kwa Wahyi, wala mimi si chochote ila ni mwonyaji mwenye kudhihirisha wazi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, uwambie washirikina wa watu wako, “Sikuwa ni wa mwnzo wa wajumbe wa Mwenyezi Mungu kwa viumbe Wake. Na sijui Atakalofanya Mwenyezi Mngu kwangu wala kwenu hapa duniani. Sifuati katika yale ninayowaamrisha nyinyi na katika yale ninayoyafanya isipokuwa wahyi wa Mwenyezi Mungu Anaoniletea mimi. Na sikuwa mimi isipokuwa ni mwenye kuonya ambaye uonyaji wake uko wazi.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس