يَمُنُّونَ عَلَيۡكَ أَنۡ أَسۡلَمُواْۖ قُل لَّا تَمُنُّواْ عَلَيَّ إِسۡلَٰمَكُمۖ بَلِ ٱللَّهُ يَمُنُّ عَلَيۡكُمۡ أَنۡ هَدَىٰكُمۡ لِلۡإِيمَٰنِ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Wanakusimbulia kuwa wamesilimu! Sema: Msinisimbulie kwa kusilimu kwenu. Bali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kufanyieni hisani kwa kukuongoeni kwenye Imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa Mabedui wanakusimulia wewe, ewe Nabii, kusilimu kwao, kukufuata wewe na kukunusuru. Waambie, «Msinisimulie mimi kuingia kwenu kwenye Uislamu, kwani manufaa yake yanawarudia nyinyi wenyewe. Na Mwenyezi Mungu Ndiye Aliyewafadhili nyinyi kwa kuwaafikia kumuamini Yeye na Mtume Wake, iwapo nyinyi ni wakweli katika kuamini kwenu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس