لِّكَيۡلَا تَأۡسَوۡاْ عَلَىٰ مَا فَاتَكُمۡ وَلَا تَفۡرَحُواْ بِمَآ ءَاتَىٰكُمۡۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخۡتَالٖ فَخُورٍ
Ili msihuzunike kwa kilicho kupoteeni, wala msijitape kwa alicho kupeni. Na Mwenyezi Mungu hampendi kila anaye jivuna akajifakhirisha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ili msisikitike kwa mlichokikosa cha ulimwengu na msifurahike furaha ya kiburi na majivuno. Na mwenyezi mungu Hampendi kila mwenye kujiona kwa alichopewa cha ulimwengu, mwenye kujifahiri nacho juu ya wengine.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس