وَمَآ أَفَآءَ ٱللَّهُ عَلَىٰ رَسُولِهِۦ مِنۡهُمۡ فَمَآ أَوۡجَفۡتُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ خَيۡلٖ وَلَا رِكَابٖ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يُسَلِّطُ رُسُلَهُۥ عَلَىٰ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Na mali aliyo leta Mwenyezi Mungu kwa Mtume wake kutoka kwao hamkuyakimbilia mbio kwa farasi wala ngamia. Lakini Mwenyezi Mungu huwapa mamlaka Mitume wake juu ya wowote awatakao. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na yale mali ya Mayahudi wa Banū al- Nadīr ambayo Mwenyezi Mungu Amewaletea, hamkupanda farasi wala ngamia ili myapate, lakini Mwenyezi Mungu Anawapa nguvu wajumbe Wake juu ya anayemtaka miongoni mwa maadui Wake, wakajisalimsha bila ya vita. (Mali hayo yanaitwa fay’), na fay’ ni mali yaliyochukuliwa kwa makafiri kwa haki bila ya vita. Na Mwenyezi Mungu kwa kila jambo ni Muweza, hakuna kitu chochote kinachomshinda.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس