رَّسُولٗا يَتۡلُواْ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ مُبَيِّنَٰتٖ لِّيُخۡرِجَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ مِنَ ٱلظُّلُمَٰتِ إِلَى ٱلنُّورِۚ وَمَن يُؤۡمِنۢ بِٱللَّهِ وَيَعۡمَلۡ صَٰلِحٗا يُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ قَدۡ أَحۡسَنَ ٱللَّهُ لَهُۥ رِزۡقًا
Mtume anaye kusomeeni Aya za Mwenyezi Mungu zinazo bainisha, ili kuwatoa walio amini na wakatenda mema kutoka gizani kuwapeleka kwenye nuru. Na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu, na akatenda mema, atamwingiza katika Bustani zipitazo mito kati yake, wadumu humo milele. Mwenyezi Mungu amekwisha mpa riziki nzuri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ukumbusho huu ni Mtume anayewasomea nyinyi aya za Mwenyezi Mungu zinazowafafanulia haki kwa kuitenga na ubatilifu, ili Apate kuwatoa, wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakazifuata Sheria Zake kivitendo na wakamatii, kutoka kwenye giza la ukafiri kuwapeleka kwenye mwangaza wa Imani. Na yoyote atakayemuamini Mwenyezi Mungu na akafanya matendo mema Atamuingiza kwenye mabustani ya Peponi ambayo chini ya miti yake inapita mito ya maji, wasalie humo milele. Kwa hakika Mwenyezi Mungu Ameifanya riziki ya Muumini mwema iwe nzuri huko Peponi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس