مَٰلِكِ يَوۡمِ ٱلدِّينِ
Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Yeye, kutakasika ni Kwake, Peke Yake Ndiye Mwenye mamlaka ya Siku ya Kiyama, nayo ni Siku ya Malipo kwa matendo yaliyofanywa na waja. Muislamu anapoisoma aya hii katika kila rakaa, inamkumbusha siku ya Akhera na inamhimiza ajitayarishe kufanya matendo mema na kujiepusha na maasia na mabaya.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس