يَوۡمَئِذٖ يُوَفِّيهِمُ ٱللَّهُ دِينَهُمُ ٱلۡحَقَّ وَيَعۡلَمُونَ أَنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡحَقُّ ٱلۡمُبِينُ
Siku hiyo Mwenyezi Mungu atawapa sawa sawa malipo yao ya haki, na watajua kwamba hakika Mwenyezi Mungu ndiye Haki Iliyo Wazi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Katika siku hiyo, Mwenyezi Mungu Atawalipa malipo yao kamili juu ya matendo yao kwa usawa, na watajua kwenye mkusanyiko huo mkubwa wa kisimamo kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Ukweli ulio wazi, Ambaye Yeye ni kweli, ahadi yake ni ya kweli, makemeo yake ni kweli na kila kitu kitokanao na yeye ni kweli, Ambaye hamdhulumu yoyote chochote hata kama ni kadiri ya uzani wa chungu mdogo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس