وَلَقَدۡ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكُمۡ ءَايَٰتٖ مُّبَيِّنَٰتٖ وَمَثَلٗا مِّنَ ٱلَّذِينَ خَلَوۡاْ مِن قَبۡلِكُمۡ وَمَوۡعِظَةٗ لِّلۡمُتَّقِينَ
Na kwa yakini tumekuteremshieni Ishara zilizo wazi na mifano kutokana na walio tangulia kabla yenu na mawaidha kwa wachamngu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kwa hakika tumewateremshia, enyi watu, aya za Qur’ani zikiwa ni dalili wazwazi za kuonesha haki, na ni mfano wa matukio ya ummah uliopita wa Waumini kati yao na makafiri na yaliyowapitia ya kuwafaa na kuwadhuru ambayo ni mfano na mazingatio kwenu na ni mawaidha ya kuwaidhika mwenye kumcha Mwenyezi Mungu na kujihadhari na adhabu Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس