وَإِذَا دُعُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَهُمۡ إِذَا فَرِيقٞ مِّنۡهُم مُّعۡرِضُونَ
Na wanapo itwa kumuendea Mwenyezi Mungu na Mtume wake ili ahukumu baina yao, kipo kikundi katika wao kinakataa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wanapoitwa, wanapokuwa kwenye ugomvi baina yao, kwenye hukumu iliyo ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu na waje kwa Mtume ili afanye uamuzi kati yao, ghafula hujitokeza kikundi kati yao kikajiepusha na kikawa hakikubali hukumu ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, pamoja na kuwa hiyo ndiyo haki isiyo na shaka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس